Mtuhumiwa wa mauaji ya watu 50 kwenye mashambulizi ya misikiti miwili mwezi uliopita nchini New Zealand ameamriwa kupimwa akili.
Kwa mujimu wa Jaji wa Mahakama Kuu, Cameron Mander, mtuhumiwa huyo atapimwa na madaktari bingwa wa afya ya akili ili kuamua iwapo anaweza kuendelea na kesi hiyo ama ni mgonjwa wa akili.
Mtuhumiwa huyo anakabiliwa na mashtaka 50 ya mauaji na mashtaka 39 ya kujaribu kuua.
Raia wa Australia Brenton Tarrant, 28, alihudhuria kesi hiyo kwa njia ya simu ya mtandao kutokea gerezani. Chumba cha mahakama kilijaa ndugu za watu ambao waliuawa kwenye mashambulizi hayo.
Mashambulio hayo ni makubwa zaidi katika historia ya taifa la New Zealand.
Waziri Mkuu wa nchi hiyo aliiita siku ya mashambulizi kuwa ni moja ya siku za kiza zaidi kwa New Zealand.
Pia ameazimia kupiga marufuku umiliki kwa raia wa silaha zote za sampuli ya kivita.
Nini kilitokea mahakamani?
Jaji Mander ameamuru mtuhumiwa achunguzwa afya yake ya akili mara mbili ili ibainike yupo katika hali gani.
Mtuhumiwa huyo alikuwa kimya akisikiliza kwa makini kilichokuwa kikiendelea mahakamani. Hakuongea kitu.
Aliweza kuwaona jaji na wanasheria tu, kamera haikuelekezwa walipo wasikilizaji wa kesi.
Jaji ameamuru aendelee kusalia rumande mpaka pale kesi yake itakapotajwa tena Juni 14.
Related Posts
Rais Dk. Shein asisitiza wafanyakazi wa umma kufanya kazi katika mazingira mazuri
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa miongoni[...]
May 02, 2019Ibada za Kanisa Katoliki Zafutwa kwa Wiki Mbili
Ibada za Kanisa Katoliki zimefutwa kwa wiki ya pili katika mji mkuu wa Sri Lanka, Colombo, serikali[...]
May 02, 2019Wasanii Afrika Mashariki Waomboleza Msiba wa Mengi
Kundi la wasanii wa muziki kutoka nchini Kenya Sauti Sol, limeungana na Afrika nzima kuombeleza msi[...]
May 02, 2019Jeshi la Polisi Lafunguka Kuhusu Kutangaza Nafasi za Ajira
Jeshi la Polisi limesema kuwa halijatangaza nafasi za ajira katika chombo chochote cha habar[...]
May 02, 2019Freeman Mbowe amlilia Dkt.Reginald Mengi
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametuma salamu pole kufuat[...]
May 02, 2019Kikosi cha Yanga SC kitakachocheza na Tanzania Prisons leo
Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (TPL) kuendelea tena leo ambapo Yanga SC watacheza dhidi ya Tanzania Pr[...]
May 02, 2019
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.