Kundi la wasanii wa muziki kutoka nchini Kenya Sauti Sol, limeungana na Afrika nzima kuombeleza msiba wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Dr. Reginald Mengi.
Sauti Sol wameeleza namna ambavyo Afrika imepoteza mtu muhimu aliyesimama kama mtu mwenye maono, mjasiriamali, mwandishi wa vitabu pamoja na baba wa watu wengi kwa namna alivyojitoa kusaidia watu.
''Twajivunia kuwa ulikuwa baba mlezi wa wengi. Pumzika baba. Ndugu zetu wa Tanzania tuko pamoja'' wameandika Sauti Sol.
Pia wameungana na wasanii wenzao wa Tanzania ambao nao wameguswa na msiba huo na kwa pamoja wametoa salamu za rambirambi kwa kueleza msaada wa Dr. Mengi katika kiwanda cha muziki na burudani kwa ujumla.
Wasanii Alikiba, Shetta, Lady Jay Dee, Nandy, Ruby, Fid Q, Billnass, Barnaba pamoja na wengine wengi wameguswa na msiba huku wakitumia mitandao ya kijamii kutuma salamu za rambirambi.
Kwa upande wake msanii Mwana FA ambaye pia ni mjumbe wa Bodi ya Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), ameeleza haya, ''Ukapumzike kwa amani mzee wetu. Umetekeleza kilichokuleta Duniani,na tumeona. Umeacha alama''.
Related Posts
Rais Dk. Shein asisitiza wafanyakazi wa umma kufanya kazi katika mazingira mazuri
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa miongoni[...]
May 02, 2019Ibada za Kanisa Katoliki Zafutwa kwa Wiki Mbili
Ibada za Kanisa Katoliki zimefutwa kwa wiki ya pili katika mji mkuu wa Sri Lanka, Colombo, serikali[...]
May 02, 2019Jeshi la Polisi Lafunguka Kuhusu Kutangaza Nafasi za Ajira
Jeshi la Polisi limesema kuwa halijatangaza nafasi za ajira katika chombo chochote cha habar[...]
May 02, 2019Freeman Mbowe amlilia Dkt.Reginald Mengi
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametuma salamu pole kufuat[...]
May 02, 2019Kikosi cha Yanga SC kitakachocheza na Tanzania Prisons leo
Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (TPL) kuendelea tena leo ambapo Yanga SC watacheza dhidi ya Tanzania Pr[...]
May 02, 2019
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.