Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametuma salamu pole kufuatia kifo cha Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt.Reginald Mengi kilichotokea usiku wa kuamkia leo mjini Dubai, Falme za Kiarabu. Chini ni taarifa ya kiongozi huyo.
Nimepokea kwa majonzi makubwa sana kifo cha Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dkt. Reginald Abraham Mengi, natuma salamu za pole kwa Watanzania na Wana- Afria Mashariki wote, hususani tasnia ya habari, michezo, wafanyabiashara, wafanyakazi wa Kampuni ya IPP, ndugu jamaa na marafiki.
Hakika Taifa limepoteza mtu muhimu sana, aliyejitoa kusaidia Watanzania wenzake katika mambo mengine. Ni kipindi kigumu kuliko wakati mwingine wowote katika maisha ya mwanadamu.
Reginald Abraham Mengi, hakika Taifa litakukumbuka ukiwa mmoja wa watu walioleta mapinduzi katika sekta ya habari na mambo mengine mengi ambayo yatafanya usiweze kusahaulika.
Kimwili haupo nasi lakini hakika matendo yako yataishi kwenye mioyo ya Watanzania. Wewe umekuwa mfano wa kuigwa, hakika tutakukumbuka.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa, Jina lake lihimidiwe.Upumzike kwa amani Dkt Reginald Abraham Mengi. We will mourn, until we join you Hero. Mwisho.
Mwenyekiti Mtendaji wa makampuni ya IPP, Dkt. Reginald Mengi amefariki dunia, kwa mujibu wa taarifa kutoka vyombo vya habari alivyokuwa anavimiliki. Mengi ambaye ni mmoja kati ya wafanyabishara wakubwa Tanzania amefariki usiku wa kuamkia leo Alhamisi akiwa Dubai.
Related Posts
Rais Dk. Shein asisitiza wafanyakazi wa umma kufanya kazi katika mazingira mazuri
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa miongoni[...]
May 02, 2019Ibada za Kanisa Katoliki Zafutwa kwa Wiki Mbili
Ibada za Kanisa Katoliki zimefutwa kwa wiki ya pili katika mji mkuu wa Sri Lanka, Colombo, serikali[...]
May 02, 2019Wasanii Afrika Mashariki Waomboleza Msiba wa Mengi
Kundi la wasanii wa muziki kutoka nchini Kenya Sauti Sol, limeungana na Afrika nzima kuombeleza msi[...]
May 02, 2019Jeshi la Polisi Lafunguka Kuhusu Kutangaza Nafasi za Ajira
Jeshi la Polisi limesema kuwa halijatangaza nafasi za ajira katika chombo chochote cha habar[...]
May 02, 2019Kikosi cha Yanga SC kitakachocheza na Tanzania Prisons leo
Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (TPL) kuendelea tena leo ambapo Yanga SC watacheza dhidi ya Tanzania Pr[...]
May 02, 2019
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.