SIKU chache baada ya mwanamitindo maarufu Bongo, Hamisa Mobeto kukutwa na skendo ya kufumaniwa na bwana wa mtu ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sasa, mwenyewe ameibuka na kukoleza fumanizi lake hilo, Risasi Mchanganyiko linakupa habari kamili.
Mobeto alidaiwa kufumaniwa na bwana wa mrembo anayejulikana kwa jina la Tahiya ambaye aliposti picha ya Mobeto kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuandika maneno haya; “Hamisa Mobeto achana na wanaume za watu.”
Baada ya muda mwanadada huyo akaposti tena meseji zao zote alizokuwa wakijibizana na mwanamitindo huyo kwenye mtandao wa WhatsApp ambapo Tahiya alionekana akimsihi Mobeto aachane na mpenzi wake lakini haikusaidia kwani mwisho wa waliishia kujibizana maneno mabaya huku kila mmoja akijiona anaweza zaidi ya mwenzake.
MOBETO AKOLEZA SKENDO
Baada ya skendo hiyo kutikisa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, Risasi liliamua kumtafuta Mobeto ambaye alilikoleza fumanizi hilo kwa kutoa maneno ya shombo.
“(Kwa sauti ya ukali) Mnataka niwaambie nini, mlichokiona ndiyo hichohicho isitoshe mimi siyo mtoto mdogo kwa hiyo naelewa ninachokifanya, sijaiba mwanaume wa mtu ila alikuja mwenyewe na nampenda nifanyeje sasa,” aliongea Mobeto na kukata simu.
Kwa upande wa mama mzazi wa Mobeto, Shufaa Lutiginga alipotafutwa ili azungumzie kuhusu skendo hiyo ya mwanaye kufumaniwa na bwana wa mtu alilipuka na kusema mwanaye aachwe aishi anavyopenda mwenyewe.
“Jamani nilishawaambia muacheni Hamisa aishi vile ambavyo yeye anapenda, msimfuatilie siku akihitaji kuongea na nyie atawatafuta yeye mwenyewe lakini siyo kila kukicha kumfuatilia,” alisema mama Mobeto
Related Posts
Rais Dk. Shein asisitiza wafanyakazi wa umma kufanya kazi katika mazingira mazuri
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa miongoni[...]
May 02, 2019Ibada za Kanisa Katoliki Zafutwa kwa Wiki Mbili
Ibada za Kanisa Katoliki zimefutwa kwa wiki ya pili katika mji mkuu wa Sri Lanka, Colombo, serikali[...]
May 02, 2019Wasanii Afrika Mashariki Waomboleza Msiba wa Mengi
Kundi la wasanii wa muziki kutoka nchini Kenya Sauti Sol, limeungana na Afrika nzima kuombeleza msi[...]
May 02, 2019Jeshi la Polisi Lafunguka Kuhusu Kutangaza Nafasi za Ajira
Jeshi la Polisi limesema kuwa halijatangaza nafasi za ajira katika chombo chochote cha habar[...]
May 02, 2019Freeman Mbowe amlilia Dkt.Reginald Mengi
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametuma salamu pole kufuat[...]
May 02, 2019Kikosi cha Yanga SC kitakachocheza na Tanzania Prisons leo
Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (TPL) kuendelea tena leo ambapo Yanga SC watacheza dhidi ya Tanzania Pr[...]
May 02, 2019
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.