KUNA baadhi ya watu kusafiri mara kwa mara siyo ishu sana, lakini kwa upande wa mrembo wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe, safari zake zimeshtua wengi, Risasi Mchanganyiko limedokezwa.
Mrembo huyo safari zake zimeshtua kutokana na jinsi ambavyo amekuwa na idadi kubwa ya picha za mara kwa mara anazotupia akiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Instagram na kurasa nyingine, wadau mbambali walirudia kuziposti (re-post) huku kila mmoja akieleza la kwake kuonesha kushtushwa kwake.
“Mh! Haiwezekani, angalia hizi picha alizoziposti mwishoni mwa wiki (iliyopita), juzi tena akaposti na leo kaposti, jamani hata kama ni jeuri ya pesa kiasi gani, hii haiwezekani,” alichangia mmoja wa wafuasi wake wapatao milioni 4.3. Mwingine alikwenda mbele zaidi, kwa kuhoji kuwa isije ikawa mrembo huyo anakwenda tu kupiga picha uwanjani hapo akiwa na mabegi yake ya nguo kisha hasafiri.
“Jamani isije mkawa mnaona anaposti tu picha airport (uwanja wa ndege) kumbe hasafiri maana haya mambo wasanii nao hawashindwi,” alichangia mfuasi mwingine. Mbali na hao, wengine walihoji zaidi kuhusu safari hizo kwa kutaka kujua ni nini kinampeleka huko China anakodaiwa kwenda mara kwa mara.
Walihoji anapata wapi pesa za kusafiri mara kwa mara wakati kazi ya uigizaji kwa sasa hailipi kama ilivyokuwa miaka ya nyuma. “Bongo Movies ya sasa kama unavyoona, sasa huyu dada atakuwa anapata wapi pesa hizi za kusafiri kila siku?” Alihoji mfuasi anayejiita Kitoi katika Mtandao wa Instagram.
Risasi Mchanganyiko lilifanya jitihada za hali na mali kumpata Wolper ili aweze kuzungumzia picha hizo na safari zake, lakini hakupatikana kirahisi. Hata hivyo, mtu mmoja wa karibu na Wolper aliyeomba hifadhi ya jina alisema anavyomjua Wolper picha anazoweka mara kwa mara huwa si za wakati husika na hicho ndicho kinachowachanganya watu washindwe kumuelewa.
“Wolper hizi safari unaweza kuta kasafiri kwa miezi tofauti mwaka jana au hata mwaka juzi halafu akawapostia mfululizo leo na watu wakashindwa kuelewa,” alisema mtu huyo. Hata hivyo, gazeti hili linaendelea na jitihada za kumpata Wolper ili lkupata undani wa safari zake za China.
Related Posts
Rais Dk. Shein asisitiza wafanyakazi wa umma kufanya kazi katika mazingira mazuri
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa miongoni[...]
May 02, 2019Ibada za Kanisa Katoliki Zafutwa kwa Wiki Mbili
Ibada za Kanisa Katoliki zimefutwa kwa wiki ya pili katika mji mkuu wa Sri Lanka, Colombo, serikali[...]
May 02, 2019Wasanii Afrika Mashariki Waomboleza Msiba wa Mengi
Kundi la wasanii wa muziki kutoka nchini Kenya Sauti Sol, limeungana na Afrika nzima kuombeleza msi[...]
May 02, 2019Jeshi la Polisi Lafunguka Kuhusu Kutangaza Nafasi za Ajira
Jeshi la Polisi limesema kuwa halijatangaza nafasi za ajira katika chombo chochote cha habar[...]
May 02, 2019Freeman Mbowe amlilia Dkt.Reginald Mengi
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametuma salamu pole kufuat[...]
May 02, 2019Kikosi cha Yanga SC kitakachocheza na Tanzania Prisons leo
Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (TPL) kuendelea tena leo ambapo Yanga SC watacheza dhidi ya Tanzania Pr[...]
May 02, 2019
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.