Binolonan ambacho ni Kijiji kinachopatikana kaskazini mwa mji mkuu wa Ufilipino, Manila, kimepiga marufuku kufanya umbea.
Meya wa mji, Ramon Guico, amesema umbea ulisababisha ugomvi mkubwa utokee katika kijiji hicho kitu kilichopelekea vikao vya viongozi kuchukua tahadhari kwa kupiga marufuku kufanya umbea.
Guico alisema kuna umbea wa aina nyingi, lakini katika kijiji hicho kesi nyingi ni za umbea unaohusu mali, pesa na mahusiano.
Sababu ya marufuku hio ni kukumbusha kwamba kila mtu na hasa wanaoishi katika kijiji hicho anawajibika kwa atakayoyasema.
Pia wanataka kuonyesha watu wengine kwamba watu wa Binolonan ni watu wazuri na eneo hilo ni salama.
Guico, aliongeza kwamba hatua walizochukua zitaongeza ubora wa kijiji hicho.
Guico aliongeza kwamba maeneo ambayo watu wake hawafanyi umbea yana Baraka zaidi, kwa sababu yeye anaamini watu wana kazi za muhimu zaidi za kufanya badala ya kufanya umbea.
Kwa mujibu wa sheria atakayekutwa na hatia ya kufanya na kueneza umbea na maneno ya uongo atatozwa faini pesa taslimu peso 200 takribni dola za kimarekani 4. Pamoja na tozo hilo la pesa atapewa adhabu ya kukusanya takataka kwa masaa 3.
Atakayekutwa na hatia ya kufanya umbea kwa mara ya pili atatozwa faini ya pesa taslimu peso 1000 takriban dola 20, faini hiyo itaambatana na kupewa adhabu ya kutoa huduma kwa jamii kwa masaa 8.
Home
»
udaku
» Kijiji Chapiga Marufuku Umbea ....Ukikamatwa Unapiga Umbea Faini Yake ni USD Dola 4 sawa na Tsh. 9200
Related Posts
Rais Dk. Shein asisitiza wafanyakazi wa umma kufanya kazi katika mazingira mazuri
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa miongoni[...]
May 02, 2019Ibada za Kanisa Katoliki Zafutwa kwa Wiki Mbili
Ibada za Kanisa Katoliki zimefutwa kwa wiki ya pili katika mji mkuu wa Sri Lanka, Colombo, serikali[...]
May 02, 2019Wasanii Afrika Mashariki Waomboleza Msiba wa Mengi
Kundi la wasanii wa muziki kutoka nchini Kenya Sauti Sol, limeungana na Afrika nzima kuombeleza msi[...]
May 02, 2019Jeshi la Polisi Lafunguka Kuhusu Kutangaza Nafasi za Ajira
Jeshi la Polisi limesema kuwa halijatangaza nafasi za ajira katika chombo chochote cha habar[...]
May 02, 2019Freeman Mbowe amlilia Dkt.Reginald Mengi
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametuma salamu pole kufuat[...]
May 02, 2019Kikosi cha Yanga SC kitakachocheza na Tanzania Prisons leo
Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (TPL) kuendelea tena leo ambapo Yanga SC watacheza dhidi ya Tanzania Pr[...]
May 02, 2019
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.