0
Ikiwa ni siku chache zimepita baada ya staa wa Bongo Fleva Ben Pol kutangaza kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake Anerlisa Muigai kutokea nchini Kenya, sasa inaelezwa kuwa wawili hao wanatarajia kupata watoto mapacha.

Taarifa hizo njema zimetolewa na Anerlisa kupitia insta story yake ambapo aliandika “Nina sali ili mapacha wafanane na wewe” . Lakini kwa upande wa Ben Pol tayari ana mtoto mmoja wa kiume aliyezaa na mpenzi wake wa zamani anayefahamika kama Latifa.

Post a Comment

 
Top