0

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Juu Hispania amewasomea hukumu viongozi 13 wakubwa wa Jimbo la Catalonia nchini Hispania, wakikabiliwa na mashtaka ya uasi juu ya majukumu yao katika kura ya maoni na tamko la uhuru mwaka 2017.

Jaji huyo Pablo Llarena amewahukumu miaka 30 jela viongozi hao ikiwa ni pamoja na Rais Mstaafu wa Jimbo hilo Carles Puigdemont na Jordi Turul ambaye kesho anatarajiwa kupigiwa kura ya kuchukua nafasi hiyo.

Ameeleza kuwa viongozi hao kwa kushirikiana na vikundi vya asasi za kijamii kwa miaka sita iliyopita wamefanya njama kusuka mpango wa kutangaza Uhuru wa Catalonia, jambo lililo kinyume na utaratibu wa kisheria nchini Hispania.

Mahakama imetoa hukumu hiyo leo March 23, 2018 na kusema kwa ujumla imetoa hukumu hiyo kwa makosa ya kuasi, rushwa na kutotii kwa viongozi hao.

Post a Comment

 
Top