0
Shilole Amkana Uchebe "Sina Mimba ya Uchebe"
Msanii wa muziki Bongo, Shilole amedai kuwa hana ujauzito wa mumuwe Uchebe kama watu wanavyomdhania baada ya kumuona amenenepa sana hivi karibuni.


Mrembo huyo amesema hayo kupitia kipindi cha Leo Tena na kudai kuwa mume aliyenaye anamfanya anenepe. “Sina Ujauzito, ila watu wananiombea mema, mume niliyenaye ananifanya ninenepe,” amesema Shilole huku akiwa na mumuewe kwenye kipindi hicho.

Akongeza kuwa dada yake alimkataza yeye kuolewa na Uchebe. “Dada alimkataa Uchebe kwa sababu anaonekana hana kipato kikubwa.”

Kwa mujibu wa wapenzi hao wamedai kuwa walikutana kisiwani Zanzibar na huki ndiko mapenzi yao yalipoanzia baada ya Uchebe ambaye ni mumuwe kuamua kueleza hisia zake.

Post a Comment

 
Top