Rais wa Liberia na nyota wa zamani wa soka George Weah, amerejea tena kazini , wiki mbili kamili baada ya kuitoroka ofisi yake kwasababu nyoka wawili walikuwa wamepatikana katika jengo la ofisi yake.
Jengo hilo lilitakiwa kusafishwa vizuri kwa kemikali ya kuua nyoka kabla rais kushauriwa kurejea ofisini kwake Jumatano.
Mmoja wa watu wa kwanza kumtembelea rais Weah katika ofisi yake alikuwa ni Makamu rais wa zamani Joseph Boakai, aliyeshindwa na Weah katika uchaguzi wa urais wa mwaka 2017.
Bwana Weah alizungumzia juu ya juhudi za serikali yake za ''kulinda misingi ya demokrasia'', na kuwavutia wawekezaji wa kigeni iki kuinua uchumi, taarifa hiyo ilitumwa kwenye wavuti wa serikali.
Rais amekuwa akifanyia kazi katika ofisi iliyopo ghorofa ya sita ya jengo la Wizara ya mambo ya nje tangu jengo jirani na ofisi ya rais lilipoungua kwa moto mwaka 2006.
Nyoka wawili weusi ambao walitoka kwenye shimo lilolokuwa kwenye sehemu ya mapokezi ya jengo la ghorofa sita walikwenda nyuma ya jengo hilo ghafla wakati watu walipokuwa wakijaribu kuwauwa.
Baada ya tukio hilo maafisa wa polisi na maafisa wa usalama wa rais walionekana wakiyalinda makao ya Bwana Weah katika mji mkuu wa Monrovia.
Nyoka wamfurusha rais wa Liberia kutoka afisini mwake
Weah atoa sheria ya 'kibaguzi' ya uraia
Wenger apatwa na mtego wa habari za uzushi
Kanda ya video iliochapishwa katika ukurasa wa kwanza wa gazeti la African News ilionyesha wafanyikazi wakijaribu kushambulia nyoka wakati walipoonekana katika eneo la kukaribisha wageni la jengo hilo.
Jumba hilo limekuwa katika eneo hilo kwa miaka kadhaa sasa kwasababu yamfumo wa maji taka , na maafisa wanasema kuna uwezekano wa nyoka kuingia katika jumba hilo.
Haijafahamiika ikiwa nyoka hao waliuawa au la.
Related Posts
Rais Dk. Shein asisitiza wafanyakazi wa umma kufanya kazi katika mazingira mazuri
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa miongoni[...]
May 02, 2019Ibada za Kanisa Katoliki Zafutwa kwa Wiki Mbili
Ibada za Kanisa Katoliki zimefutwa kwa wiki ya pili katika mji mkuu wa Sri Lanka, Colombo, serikali[...]
May 02, 2019Wasanii Afrika Mashariki Waomboleza Msiba wa Mengi
Kundi la wasanii wa muziki kutoka nchini Kenya Sauti Sol, limeungana na Afrika nzima kuombeleza msi[...]
May 02, 2019Jeshi la Polisi Lafunguka Kuhusu Kutangaza Nafasi za Ajira
Jeshi la Polisi limesema kuwa halijatangaza nafasi za ajira katika chombo chochote cha habar[...]
May 02, 2019Freeman Mbowe amlilia Dkt.Reginald Mengi
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe ametuma salamu pole kufuat[...]
May 02, 2019Kikosi cha Yanga SC kitakachocheza na Tanzania Prisons leo
Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (TPL) kuendelea tena leo ambapo Yanga SC watacheza dhidi ya Tanzania Pr[...]
May 02, 2019
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.