0
Gigy Money ameonyesha kutokubaliana na utaratibu wa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) uliowataka ma-video vixen kujisajili katika Baraza hilo.

Muimbaji huyo ameiambia XXL ya Clouds Fm kuwa Basata walimueleza hilo lakini anaona kuna ma-video vixen wengi ambao hawajasalijiwa na wanafanya kazi hiyo.

“Waliniambia hivyo, lakini sasa Hamisa Mobetto anafanya nini, Tunda tuseme anafanya nini, officialnai anafanya nini, ma-video vixen unataka kuniambia wanajulikana Basata, why Gigy kwa sababu umeonekana ashapata chochote kitu,” amesema Gigy Money.

“Basata mtajalije utamaduni wa msanii mkiwa hamjali Ugali wake, haujali mfuko wake, wewe unaniona tu napendeza unajua mimi napoteza shilingi ngapi,”

Gigy Money kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Mimina baada ya kutamba na ngoma ‘Papa’.

Post a Comment

 
Top