0
Akiongea na kituo cha Taifa cha Utangazaji(TBC),Mbunge wa Bumbuli na Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano,Ndugu January Makamba,amesema katika uchaguzi wa mwaka 2015 CCM ilikuwa inaondoka madarakani kwa nguvu ya wananchi,lkn kwa uchaguzi wao wa kumchagua ndugu JPM kidogo imani ya wananchi ikarudi kwa Chama Cha Mapinduzi.

Makamba Jnr anasema CCM ilipoteza imani na kutoaminiwa na wananchi kwa kiasi kikubwa sana kiasi cha wao kuona dalili la wazi la kuanguka kwa CCM.Anasema uchaguzi wa 2015 ulikuwa ni moja ya chaguzi ngumu kuwahi kutokea na wana imani kwa utendaji huu wa JPM wananchi watarudisha imani kwa CCM na Serikali yake na kuepuka kuwaadhibu ktk sanduku la kura mwaka 2020.

Post a Comment

 
Top